Powered By Blogger

Friday, June 10, 2011

MUME WA MTU NA MATATIZO YAKE

HEBU SOMA STORY YA HUYU DADA.
Story nimeipata jamiiforums. watu wengi wamechangia kwa mitazamo tofauti. Wewe unasemaje?
 
NATAMANI KUJIUA:
stock photo : Portrait of young African American woman smiling isolated over white background
Habari zenu wana Jamii Forum. Mimi ni mgeni humu. Ila si mgeni ki hivyo nimekuwa natembelea bila kuwa member. Nimeamua kujiunga ili nipate kushauriwa kwani shida niliyonayo siwezi kushare na mtu ninaye mjua.Mimi ni mdada wa miaka 32. Ni mrembo sana yaani wale mnaoita 8 figure. Sijisifii ila hilo nimeona nilitamke ili muweze kuielewa vizuri mada yangu.

Nilitokea kumpenda sana kijana mmoja na kuja kugundua baada ya miezi miwili kuwa ni mume wa mtu. Kaka ni muislamu hivyo havai pete na kwa kuwa ni kijana sikuweza kudhania kuwa ni mume wa mtu na kwa kweli ningejua nisinge mpa moyo wangu.
Tatizo niligundua kuwa kaoa wakati nimeshampenda. Na ni yeye mwenyewe alinitamkia kuwa nina mke baada ya kujua sitaweza kumwacha kwani nilikuwa nimekolea. Tumekaa kwenye uhusiano kwa muda wa mwaka na nusu sasa mpaka pale mkewe alipokuja kugundua. Mimi mkewe nilikuwa nimeshamjua. Ni mdada msomi na ana kazi nzuri sana ila ni wa kawaida na aniingii hata nusu kwa uzuri kwa hiyo nilijua tu kuwa mumewe atakuwa ananipenda mimi zaidi na labda kuna siku nitakuwa mke wa pili kwani ni muislamu.
stock photo : Portrait of Happy Smiling African American Family Isolated on White Background

Tatizo limeanza miezi miwili iliyopita. Jamaa alinipigia simu akanambia mkewe amejua kuwa tuna uhusiano, kwa hiyo mimi na yeye basi kwani hataki kuvunja ndoa yake. Nimeumia sana imagine mwaka na nusu na nimeshampenda sana. Nimejitahidi kumfuata ofisini kwao secretary wake ananambia jamaa kasafiri wakati gari naliona nje ya ofisi. Nimempigia simu simpati naona amebadili namba. Hivi kweli wanaume mnaweza kuwa wakatili hivi? Kibaya zaidi mkewe kutwa ananipigia simu na kunitisha kuwa atanifukuzisha kazi. Mimi sijali kufukuzwa kazi kwani ninampenda sana huyo mwanaume.

Nishaurini nifanyeje kwa wale wenye uzoefu wa kuwa vimada na wale wenye nyumba ndogo. Msinitukane jamani. Mimi sijawahi maishani mwangu kutembea na mume wa mtu zaidi ya huyu na sikuwahi kuwaza kuwa yatanikuta. Hivi nyie wanawake wa kwenye ndoa uwa mnawaroga wame zenu? Iweje mtu niliyekuwa nampagawisha the other day leo aseme sitaki kukuona tena kisa tu mkewe kajua? Na huyu mkewe nimfanyeje aache kunifuata fuata. Maana amekuwa ananipa vitisho kila kukicha mpaka nahofia uhai wangu. Mumewe mwenyewe kesha niacha na yeye bado analeta mikwara wakati nikimwangalia hata ngumi moja namuua.
 
MAONI YANGU:
Pole sana dada yangu. Ni kweli kuwa mambo mengi yametokea kwako mazuri na mabaya. Kwanza naomba nikutoe hofu kuwa ulikuwa umefanya kosa kupendana na huyo jamaa. your were just right. Ulimpenda kama vile ambayo ungempenda mwanaume mwingine yeyote. kwanza hukujua kama ameoa hivyo siyo kosa lako.

Pili huyo bwana pia yuko right kukuacha kwa kuwa mambo kama haya yanapofichuka huwa yana pressure sana hivyo kuendelea nawe angeendelea bila kuwa na raha yoyote. Kumbuka kuwa huyo mkewe sasa anaweza kuwa anamfuatilia mumewe pia hivyo kuna uwezekano wa kufumaniwa ambayo huyo ni aibu kubwa sana kwenye maisha ya Kiafrika.

Tatu: Unapaswa kujaribu kuondoa mawazo yako kwa huyo bwana. Futa kabisa usimuwaze kabisa. Hili najua ni gumu kwa kuwa moyo na penzi lenu lilifika mbali sana. JITAHIDI umuondoe kwenye mawazo yako na utafanikiwa. Tahadhari sana usitumie kilevi kama pombe au sigara au madawa kama njia ya kumsahau huyo bwana. Tumia njia ya kawaida tu na utafanikiwa. Jaribu pia kutumia muda mwingi sana ofisini kwa KULIKO KAWAIDA na utaona mafanikio yake.
stock photo : Young African American Woman wearing a black dress isolated on a white background
KUMBUKA: Watu wengi wanaoachwa hujitahidi kuoa, kuolewa KWA HARAKA SANA. Hilo ni moja ya makosa makubwa katika maisha. Kwa sasa jaribu kujizuia usipate mwanaume mwingine ile roho yako itulie na machungu yote yapungue. Ukipata mwingine harakaharaka kuna uwezekano mkubwa wa kuachana harakaharaka pia.
stock photo : Young beautiful black woman listening to music

USIJIUE. Maisha bado ni marefu, na matamu bila huyo bwana. Kwanza nashukuru kuwa wewe ni mrembo sana (ingawa sijakuona) na pia unajua kupagawisha kama ulivyosema mwanzo. USIJIUE tulia utapata bwana mzuri, mwema, wako 100% na utafurahia maisha siku zote za maisha yako. TULIA, VUMILIA NA BAADAYE UTAFURAHIA MAISHA UPYA KABISA. Enjoy.

No comments:

Post a Comment