Powered By Blogger

Wednesday, December 22, 2010

TAHADHARI KWA VIJANA KUTOKUNYWA POMBE NA MAPENZI KABLA YA NDOA

stock photo : Happy smiling couple in love. Over white background
Mama Kanisa anajitahidi kuwa makini, ili kuwasaidia vijana waweze kufurahia maisha ya ujana wao na hatimaye, waweze kujiandaa kikamilifu katika kutekeleza majukumu mbali mbali ndani ya familia na jamii kwa ujumla, kwa kukazia tunu na maadili mema kama msingi bora wa maisha.
 stock photo : Man with two beer mugs isolated over white baclground
Ujana ni kipindi cha mpito, lakini fainali iko uzeeni ndivyo wanavyosema waswahili. Ngono, ulevi wa kupindukia na matumizi haramu ya madawa ya kulevya ni kati ya vishawishi vikubwa vinavyoyaandama maisha ya vijana, sehemu mbali mbali za dunia. stock photo : Happy smiling man with leather trousers (lederhose) holds oktoberfest beer stein. Isolated on white background.
Baraza la Maaskofu katoliki nchini Ireland, wameandaa mbinu mkakati utakaowasaidia vijana kuepukana na madhara yanayotokana na ulevi wa kupindukia, matumizi haramu ya madawa ya kulevya na ngono kabla ya ndoa, ili kuwajengea misingi ya utu wema kuanzia sasa. Hili ni jukumu la Kanisa na Jamii kwa ujumla.
stock photo : man with bottle of beer
Familia na waamini maparokiani wametakiwa kujifunga kibwebwe ili kupambana na ulevi wa kupindukia na matumizi haramu ya madawa ya kulevya. Wazazi na jamii inafahamu mienendo ya watoto wao mtaani, wakiamua kushirikiana na Kanisa, vitendo hivi vinavyotishia uhuru, maisha na tunu bora za kikristo na kijamii vitaweza kudhibitiwa.


Wazazi wawaelimishe watoto wao kwa mifano mizuri ya maisha madhara ya ulevi wa kupindukia na ngono za utotoni. Kila kitu kina wakati wake, vijana wajifunze kuvuta subira, hata wakati mwingine wasukumwe na dhamira nyofu kusema "NO TIME".

Watoto na vijana wanayo haki ya kukua na kulelewa katika mazingira safi na salama, wakilindwa dhidi ya matumizi haramu ya madawa ya kulevya na ulevi wa kupindukia.

stock photo : Couple sitting on floor smiling in front of partially painted wall in home.
Kanisa Katoliki linaendelea kushirikiana na Serikali ya Ireland ili kufanikisha kampeni ya kuwalinda vijana dhidi ya mmong'nyoko wa maadili unaoweza kuwakumba katika hija ya maisha yao.

No comments:

Post a Comment